Kwa madhumuni ya uendeshaji wa Uchaguzi Mdogo wa Udiwani Kata ya Mzimuni wa mwaka 2026 na kwa kuzingatia masharti ya kifungu cha 6 (6) cha Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani Na. 1 ya Mwaka 2024, kikisomwa pamoja na kanuni ya 11 ya Kanuni za Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani za Mwaka 2025; pamoja na Tangazo la nafasi za kazi za muda za watendaji wa vituo vya kupigia kura kwa ajili ya uchaguzi mdogo wa Udiwani kata ya Mzimuni; lililotolewa tarehe 11 Mei, 2026; Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Kinondoni anawatangazia waombaji ambao majina yao yapo hapa chini, kufika kwenye usaili siku ya Jumatatu, tarehe 25/05/2026 katika Ukumbi wa Shule ya Sekondari Turiani kuanzia saa moja nusu (1:30) asubuhi.
Attachments